Vita ya Shetani na Mungu inatuathiri zaidi sisi wanadamu – na hapo baadaye itamuathiri Shetani pia. Vita hii haiwezi kuisha hadi siku ya mwisho, Yesu Kristo atakaporudi kuwachukua wateule wake. Pambana kwa njia ya maombi hadi siku ya mwisho kwa sababu adui tunayepambana naye hana muda wa kupumzika. Pambana kujiombea na kuwaombea wengine waliohai, na hata wale ambao bado hawajazaliwa, kabla mafuta ya dunia hii hayajalipuka. Usiishi kama adui wa msalaba wa Yesu Kristo, badala yake, ishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo. Kuishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo ni kupinga majivuno yote ya Shetani kwa upendo uliotukuka wa kujishusha au kujidharirisha, kutokutetereka hata kidogo na tamaa za ulimwengu huu kwa upendo mkubwa wa umaskini, na kutokuyumba wakati wa matatizo kwa sababu wakati wa amani ulijilimbikizia imani.
adui
amani
battle
day-of-judgement
elects
enemy
faith
fight
friend
god
humans
imani
jesus-christ
love
mafuta-ya-dunia-hii
majivuno
maombi
matatizo
msalaba-wa-yesu-kristo
mungu
needs
oil-of-this-world
pambana
peace
poverty
prayers
pride
rafiki
satan
shetani
siku-ya-mwisho
tamaa-za-ulimwengu-huu
the-cross-of-jesus-christ
the-desires-of-this-world
umaskini
upendo
vita
wanadamu
wateule
yesu-kristo
About This Quote
About Enock Maregesi
Enock Maregesi.